Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga amekutana na Wazee, Viongozi wa Dini pamoja na Vyama vya Siasa ikiwa ni kuwashukuru kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika nyanja mbalimbali katika kuhakukisha Wilaya ya Liwale inapata maendeleo.
Mheshimiwa Mlinga amewaleza wazee pamoja viongozi wa dini na vyama vya siasa miradi ya Serikali ambayo inatekelezwa hapa Wilaya ya Liwale ikiwemo ujenzi wa barabara Liwale mpaka Masasi kwa kiwango cha lami, ujenzi wa Shule na Madarasa, ujenzi wa vituo vya Afya usambazaji wa Umeme Vijijini na kuhakikisha pia Liwale inapata maji safi na salama, Mheshimiwa Mlinga amewataka wazee pamoja na viongozi wa dini na vyama vya siasa waendelee kushirikiana na Serikali ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ili wananchi wapate maendeleo.
Aidha Mheshemiwa Mlinga amewakumbusha wazee ,viongozi wa dini na vyama vya siasa kuwa ni muhumu kusimamia na kuzilinda rasilimali za Wilaya ya Liwale ili ziweze kuwanufaisha watu wa Liwale na kuleta maendeleo katika Serikali za vijiji vyetu bila usimamizi wa rasilimali hizi kama misitu tubaki kila siku tunalalamika kumbe ni sisi tumeshindwa kusimamia kikamilifu rasilimali zetu , “ kumekuwa na upotevu mkubwa wa mapato katika sekta ya misitu watu wengi wanavuna bila kufuata utaribu na sheria pia wengine wanatumia leseni ambazo sio zao katika uvunaji hivyo tumewataka wavunaji wote walipe madeni yao, pia viwanda vyote vinavyo fanya kazi nyakati za usiku nimeviagiza ni marufuku kufanya kazi usiku kwani magogo mengi ambayo ayajakaguliwa ndio yanachakatwa usiku nahili nitaendelea kulifanyia kazi kwa ukaribu zaidi naomba wazee mnipe ushirikiano”.
Kwa upande mwengine Mheshimiwa Mlinga amewakumbusha wazee na viongozi wengine kuhakikisha wana kuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanasimamia kamati za maliasili za vijiji kwani hawa ndio wamekuwa chanzo cha upotevu wa mapato ya tokanayo na misitu kwa kushirikiana na wafanyabiashara wa mbao kwani wamekuwa wakivunja utaratibu ambao umewekwa na kusababisha Serikali kupoteza mapato.
Pia Mheshimiwa Mlinga amewaeleza wazee na viongozi wa dini na vyama vya siasa kuwa Serikali imeendelea kupambana na wanyama waharibifu tembo hivi karibuni kuna mradi ambao umekuja wa GIZ ikiwa ni ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania pamoja na Serikali ya Ujerumani hii itasaidia kwa vijana wetu wa Wilaya ya Liwale kupewa mafunzo na vifaa ili kupambana na wanyama hawa waharibifu, pia awaeleza juu ya juhudi za Serikali zinazo chukuliwa katika kupambana na mifugo ikiwemo kuligawanya eneo la Kata ya Kimambi kwa wafugaji kila mfugaji apate eneo lake na kuliendeleza kwa kuchimba visima vya maji pamoja na kupanda nyasi kwenye eneo atakalo pewa na pia kuna sheria ndogo zimepitishwa katika Halmashauri ili kupambana na mifugo .
Viongozi wa dini pamoja na wazee wa Wilaya ya Liwale wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga
Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters
Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE
Simu ya Mezani: 023 2937043
Mawasiliano ya mkononi:
Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz
Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.