Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga amevifungia viwamda viwili ambavyo kuendelea na shughuli za uchakataji wa magogo baada ya kubaini kuwepo na uchakataji wa magogo ambayo ayajagongwa na pia kuchakata magogo bila kufuta utaratibu ambao upo hivyo kuisababishia Serikali na Kijiji kukosa mapato hayo yamejiri katika ziara ya Mkuu wa Wilaya katika Kijiji cha Mtawatawa.
Mheshimiwa Mlinga ameitaka Kamati ya Maliasili ya kijiji cha Mtawatawa kuhakikisha inasimamia vyema rasilimali za misitu ambayo inapatikana kijijini hapo ikiwemo kuwatambua wavunaji ambao wanatambulika na wana leseni halali na zinazo soma majina yao ili kudhibit uvunaji haramu katika kijiji cha Mtawatawa na pia aimeitaka Kamati ya maliasili kuhakikisha inafuta sheria ambazo zimewekwa na pia kuwa waadilifu ili kuisaidia Serikali pamoja na kijiji na pia kudhibiti uvunaji haramu ambao unafanywa napia kuacha kupokea rushwa kutoka kwa wafanya biashara wa magogo kwani kufanya hivyo ni kuhalalisha uvunaji haramu jambo litakalopelekea kupoteza na kufungwa kwa msitu.
Aidha Mheshimiwa Mlinga ameitaka Kamati hiyo kupeleka majina ya wavunaji wote ambao wamepitishwa na kijiji ili awatambue na kwa sababu kumekuwa na mazoe ya kutumia leseni moja kutumiwa na zaidi ya mvunaji mmoja na pia natoa agizo” Kila mvunaji atumie leseni yake ni marufuku kutumia leseni ya mtu mwingine au kampuni ambayo siyo yake kwenye uvunaji hii imepelekea kuwepo na wizi wa magogo na pia uchanaji wa mbao ambazo sio halali huu unafanywa na watu ambao hawana leseni napia mbaya zaidi mchana awafanyi kazi usiku ndio wananza kufanya kazi wakijua kuwa wakaguzi awezi kupita mda huo kwenda kuwakagua uhalali wa magogo yao yaliyopo kiwandani”.
Hata hivyo Mheshimiwa Mlinga amepongeza jitihada zinazo fanywa na Shirika la Mpingo kwa kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha litaoa mafunzo kwa vijiji katika wilaya ya Liwale katiakika kuhifadhi na kuongeza thamani ya mazo ya misitu kwa kutoa mashine za kisasa za uchakataji wa magogo, mashine za kukaushia mbao hii itasaidia vijiji kufanya biashara ya mbao na sio kuuza magogo kama awali na mapato yataongezeka kwa vijiji na Serikali
Nae mihifadhi misitu wilaya ya Liwale Richard Tarimo ametoa rai kwa wananchi wa kijiji cha Mtawatawa kuacha kuvuna miti michanga ambayo ijafikia umri wa kuvunwa kufanya hivyo kutasababisha msitu huo kufungwa na kijiji kitapoteza mapato na pia amewataka wamiliki wa viwanda vya kuchakata magogo kuhakikisha wanachakata magogo ambayo yamekaguliwa na kugongwa na kuacha kuchakata magogo ambayo uvunaji wake ni haramu na pia doria za kulinda misitu inaendelea na tunabaini watu ambao wanaingiza magogo viwandani nyakati za usiku na ambayo ayajagongwa hivyo tutashughulika nao kwenda kinyume na utaratibu.
Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga akikagua magogo ambayo yapo katika mashine za mtawatwa katika ziara yake kijijini hapo.
Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters
Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE
Simu ya Mezani: 023 2937043
Mawasiliano ya mkononi:
Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz
Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.