Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga amewewataka wafugaji wote wa Kata ya Kimambi kuhakikisha wanatumia maeneo waliyopewa kwa ajili ya ufugaji na sio kwa ajili ya shughuli za kilimo kwani kutumia maeneo ya ufugaji kwa ajili ya kilimo ndio chanzo cha migogoro kati ya wakulima na wafugaji na Mheshimiwa Mlinga amayasema hayo katika ziara yake katika Kata ya Kimambi.
Katika ziara hiyo Mheshimiwa Mlinga alianza kuongea na wazee wa Kijiji cha Kimambi na kuwasikiliza kero zao na pia katika mkutano wa hadhara wa wananchi wa Kijiji cha Kimambi Mheshimiwa Mlinga amewataka wafugaji kuafuta sheria na makubaliano ambayo wamekubalina kwani wafugaji ndio wamekuwa wavunjifu wakubwa wa sheria hivyo nilazima tufuate taratibu kwani nyie ndio mnao lalamikiwa sana kwa matendo yenu ikiwemo kulisha mifugo yenu kwenye mashamba ya watu, kuharibu vyanzo vya maji, kuharibu mindombinu.
Katika utambuzi na umiliki wa mashamba katika kijiji cha Kimambi Mheshimiwa Mlinga ameiyagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa Takukuru kufanya uchunguzi na kujua uwalali wa umiliki wa ardhi kwa watu wanao uza ardhi kwani kijiji cha kimambi kimekuwa tabia ya kuuza ardhi kiholela kwa wafugaji na kuna watu ambao wanajipatia maeneo hayo kwa njia ya udanganyifu.
Pia Mheshimiwaa Mlinga amewataka viongozi wa vijiji kuacha tabia ya kupokea rushwa kutoka kwa wafugaji kwani wao ndio wamekuwa chanzo cha mifarakano baina ya wakulima na wafugaji kwa sababu ya kutofuata taratibu za umiliki wa ardhi ambao umewekwa na kijiji na pia wananchi muache kuuza ardhi itunzeni kwa ajili ya kizazi cha kesho.
Mheshimiwa Mlinga pia amewataka wananchi wa kijiji cha kimambi kuheshimu mipaka iliyo wekwa kwani wafugaji wamekuwa wakivamia maeneo ya hifadhi ya wanyamapori Magingo kwa kupaka rangi ambayo inawapa ardhi kinyume na sheria kwani kijiji cha kimambi kimekuwa hakina uhaba wa ardhi kina eneo la kutosha hivyo tuache tabia ya kuvamia maeneo ambayo siyo ya kwetu na pia kijiji huki hakina mgogoro wa mipaka kama mnavyo dai.
Na pia Serikali itahakikisha kuwa kila mfugaji atapewa eneo lake kwa ajili ya ufugaji na hivyo anawajibu wa kuliendeleza kwa kupanda anyasi na kuchimba visima na marambo katika eneo atakalo kabidhiwa atakaye fanya kinyume na hivi basi sheria itachukua mkondo wake aidha Mheshimiwa Mlinga amewataka wafugaji kuheshimu taratibu ambazo zimewekwa na pia kuheshimu mashamba ya watu na vyanzo vya maji.
Kwa upande mwingine Mkuu wa Wilaya amewataka wananchi wa kijiji cha kimambi kuanza harambee kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya kwani kijiji cha kimambi kimekuwa na idadi kubwa ya watu hivyo nilazima huduma pia ziongozeke hivyo mnawajibu wakuanza kuchangia na kuanzisha boma na Serikali italeta pesa na kuendelea na ujenzi
Na pia miradi mingine ya maendeleo bado Serikali inaleta ikiwemo miradi ya maji, elimu, miundombinu, ya barabara, na mawasiliano hivyo tuendelee kuinga mkono Serikali ili tuweze kukamilisha lengo la kuleta maendeleo katika kijiji hichi cha Kimambi na 2qzpia wafugaji tuwapeleke watoto shule ili wapate elimu na wapate uwelewa.
Baadhi ya wazee wa kijiji cha Kimambi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga ambaye ayupo pichani.
Picha mbalimbali katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kimambi na Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Goodluck Mlinga.
Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters
Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE
Simu ya Mezani: 023 2937043
Mawasiliano ya mkononi:
Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz
Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.