Halmashauri ya Wilaya ya Liwale imeshika nafasi ya kwanza kati ya Halmashauri Sita (06) za Mkoa wa Lindi kwa kufaulisha Wanafunzi waliofanya Mtihani wa kumaliza Elimu ya Sekondari (CSEE) kwa Mwaka 2024 kwa Asilimia 98.67
Jumla ya Wanafunzi 821 kati 832(ME=451 na Ke=381) walofanya Mtihani wa kumaliza Elimu ya Sekondari(CSEE) walipata ufaulu wa Daraja la I hadi IV na Wanafunzj 11 tu ndiyo waliopata ufaulu wa Daraja la,Sifuri(0).
Halmashauri ya Wilaya ya Liwale imepokea Tuzo ya Glass kwa Kufaulisha Wanafunzi 401 kwa Daraja la I-III sawa na Asilimia 48.2.
Halmashauri ya Wilaya ya Liwale pia imepokea Tuzo ya Glass kwa kufanya vizuri katika Usimamizi na Ufuatiliaji Miradi ya Elimu
Tuzo hizi zimetolewa na Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi katika Sherehe za utoaji Tuzo za Mkoa zilizofanyika tarehe 2/5/2025 katika Viwanja vya shule ya Msingi Likangara kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa.
Sambamba na Tuzo hizo, Halmashauri imefanikiwa kutoa Mkuu wa Shule wa Mfano wa Kiongozi Bora ambaye ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Barikiwa Mwalimu Salumu Kimbendela , ambaye amefanikiwa kupandisha ufaulu kwa miaka mitatu mfululizo 2022 ikipata GPA =3.3537,2023 ikipata GPA=3.2483na 2024 ikipata GPA=3.3667.
Mwalimu Salumu Kimbende ambaye ni Mkuu Shule ya Sekondari Barikiwa na ni Mwalimu wa Somo la Bailojia amepongezwa kwa somo lake kufanya vizuri kwa ufaulu wa GPA=2.9524 Mwaka 2022,GPA=3.0370 Mwaka 2023 na GPA=3.2581 Mwaka 2024.
Katika Sherehe hizo Shule mbali mbali ,Walimu na Wanafunzi waliofanya vizuri katika Mitihani na Pimaji za Kitaifa walipokea zawadi mbalimbali..
Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters
Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE
Simu ya Mezani: 023 2937043
Mawasiliano ya mkononi:
Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz
Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.