Halmashauri ya Wilaya ya Liwale leo imetoa mafunzo ya Mfumo mpya wa manunuzi ya umma kwa njia ya mtandao NeST yaan National e procument system kwa watumishi wote ambao wanatoka katika kada ya Afya, Elimu, pamoja na Maafisa wengine ikumbukwe kuwa kuanzai octoba mosi taasisi zote za umma zitaanza kutumia mfumo huo.
Lengo la mafunzo haya ya ni kudhibiti ununuzi wa umma unao zingatia uwazi kutokana na mahitaji mapya ya teknolojia pamoja na maelekezo ya Serikali la kuimarisha eneo la ununuzi PPRA ilianza zoezi la kusanifu mfumo huo hali inayosaidia misingi mikuu ya kimataifa ya ununuzi kuzingatiwa.
Mfumo huu wa NeST utakuwa mbadala wa mfumo unao utumika sasa hivi sasa wa TANePS unatarajiwa kutatatua changamoto za kiufundi na hivyo kukidhi mahitaji ya Serikali katila sekta ya manunuzi.
Pia faida za kutumia mfumo huu wa NeST ni kuongezeka kwa uwazi na kuondoa mwingiliano wa kibinadamu na kuongeza uwajibikaji, kuhakikisha taratibu zote za manunuzi zinaweza kufanyika ndani ya mfumo.
Hivyo basi kuanzia Octoba mosi michakato yote ya zabuni za Serikali, zabuni za umma zitafanyika kupitia mfumo wa NeST na hakuna Taasisi yoyote itakayo ruhusiwa kuchakata zabuni nje ya mfumo wa NeST na pia mfumo huo umeanza kuunganishwa na mifumo mingine ikiwemo Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni BRELA Mamlaka ya Mapato TRA.
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale wakifatilia mafunzo ya mfumo mpya wa manunuzi ya umma NeST.
Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters
Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE
Simu ya Mezani: 023 2937043
Mawasiliano ya mkononi:
Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz
Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.