Mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya ya Liwale ndugu Tina Sekambo leo amekagua mradi wa Hospitali ya Wilaya ya Liwale ambapo amekagua wodi 3 ambazo ni wodi ya Mama na Mtoto, wodi ya kina Mama na wodi ya kina Baba ambapo ujenzi wake umefikia hatua za mwisho ili uweze kukamilika na kuanza kutumika.
Mkurugenzi amemuhimiza msimamizi wa ujenzi kufanya kazi kwa bidii ili mradi huo ukamilike na uwanze kutoa huduma kwa wananchi wa Liwale, ujenzi huo unagharimu kiasi cha shilingi milioni 750, 000,000,00 kutoka Serikali kuu ikiwa ujenzi wa wodi 3 na jengo la Mochwari kwakutumia njia ya ujenzi wa Force Account.
Aidha Mkurugenzi Tina Sekambo pia amekagua mradi wa Shule ya msingi Kambarage/Mbonde ukiwa una tekelezwa kupitia mradi wa Boost ambapo jumla ya shilingi milioni 331,600,000.00 zimetumika kukamilisha ujenzi ikiwa ni ujenzi wa vyumba 9 vya madarasa matundu 16, ya vyoo Jengo la utawala na kichomea taka, ambapo ujenzi huo mpaka sasa umefikia asimia 95% kukamilika.
Pia Mkurugenzi amemtaka msimamizi wa ujenzi wa Shule ya msingi Kambarage/Mbonde kuhakikisha vifaa vya ujenzi vinatumika kama ilivyo kusudiwa na ambavyo vimebaki ikiwemo rangi, malumalu, saruji na mabomba vipelekwe kwenye miradi mingine ambayo haijakamilika ili visiaharibike.
Aidha Mkurungenzi anaishukuru Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Halmashauri ya Wilaya ya Liwale fedha kwa ajili ya miradi ya Afya na Elimu ambayo inakwenda kuwasaidia wananchi wa Liwale.
Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters
Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE
Simu ya Mezani: 023 2937043
Mawasiliano ya mkononi:
Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz
Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.