Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga amefungua mafunzo ya jeshi la Akiba yenye jumla ya wanafuni 119 wanawake na wanaume kwa kundi la 10 kwa mwaka 2023 katika kata ya Liwale B.
Hayo yamejiri katika viwanja vya shule ya msingi Mkwajuni ambapo mafunzo hayo yanatolewa na kwa kujumuhisha wakufunzi 7 huku mgeni rasmi akiwa ni Mkuu wa Wilaya, akizungumza na wanafunzi hao wakati akifungua mafunzo kwa kuwapongeza mabinti walio jitoa kujiunga na jeshi la Akiba na kwataka wanafunzi hao kuwa watiifu, wakakamavu na uvumilivu kwenye kuzingatia mafunzo wanayopata.
‘’Niwapongeze mabinti ambao mmejiunga na jeshi letu la Akiba mmekuwa kipaumbele kwa msimu huu haikuwai tokea lakini pia mnapaswa kuwa watiifu na wakakamavu wakati mnapatiwa mafunzo naami uvumilivu mtaouonesha basi utawafanya mfanikiwe licha ya changamoto mbalimbali ambazo mnakabiliananazo’’.
‘’Pia nimesikia kero zenu nyie fanyenu majukumu yenu yanayotakiwa nami binafsi nawahaidi kuwasaidia ivyo amabavyo mmeviomba lakini pia ujuzi huu mnao jifunza hapa mnapaswa kuishi nao kwakulinda amani ya nchi na kutojiusisha na mambo ya rushwa kwa kupokea ama kutoa mbali na hayo changamkieni fursa ambazo zipo hapa wilayani kwetu.
Hatahivyo mshauri Mkuu wa Jeshi la Akiba Liwale Gwamaka Charles Masinde amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kuuzuria tukio hilo na kueleza mafunzo ambayo wanayotoa kwa jeshi hilo la Akiba ikiwemo elimu kuuusu vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
‘’Binafsi nikushukru Mkuu wa Wilaya na nikupongeze kwa kuudhuria ufunguzi huu ambao unausisha wanafunzi 119 kwa wanawake na wanaume, wakufunzi 7 ambao anausika moja kwa moja kutoa mafunzo licha ya kuwa tunatoa mafunzo ya kijeshi pia tunawafundisha umuhimu wa vyombo vya habari na hasara za mitandao ya kijamii’’ Ivyo mafunzo hayo yatadumu kwa miezi 6 na kumalizika mwezi 12.
Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters
Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE
Simu ya Mezani: 023 2937043
Mawasiliano ya mkononi:
Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz
Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.