Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga ametembelea na kukagua Shule za Msingi Wilaya ya Liwale ambazo zinajiaanda na mtihani wa kuhitimu Elimu ya Msingi ambapo jumla ya shule 65 za msingi, zitafanya mitihani hiyo huku idadi ya wanafunzi ikiwa ni jumla 2216, wavulana 1029 na wasichana 1187.
Mheshimiwa Mlinga amewapongeza walimu na wanafunzi kwa maandalizi mazuri ya mtihani wa kumaliza darasa la saba na kuwatia moyo “kuwa hapo ndio mwanzo wa safari yao ya maisha na elimu hivyo amewasisitiza wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao ili waweze kufaulu na kuendelea na masomo ya elimu ya sekondari , kwani kusoma ndio ambako kutawakomboa na sio vinginevyo” pia Mkuu wa Wilaya amewapa kalamu moja moja wanafunzi wote katika Wilaya ya Liwale.
Aidha Mkuu wa Wilaya ametoa rai kwa wazazi wote kuhakikisha wanawasimamia watoto wao katika kuhakikisha wanapata elimu na kudhibiti utoro mashuleni na wazazi ambao watakikuka taratibu basi sheria itachukuliwa dhidi yao.
Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga akikagua Shule za Msingi ambazo zinajiandaa na mitihani ya kuhitimu Elimu ya msingi.
Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters
Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE
Simu ya Mezani: 023 2937043
Mawasiliano ya mkononi:
Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz
Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.