• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Liwale District Council
Liwale District Council

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Uhasibu
      • Miundo Mbinu
      • Afya
      • Usafishaji na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Mifugo
    • Vivutio vya kitalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Ugani
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Uchumi na Mazingira
      • Community Services
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Miongozo mbalimbali
  • KItuo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi na kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

TANGAZO LA KAZI IDARA YA AFYA HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE

06 March 2023

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale anakaribisha maombi ya Watanzania wenye sifa na uwezo wa kujaza nafasi za Kazi za Mteknolojia Dawa Msaidizi kama ifuatavyo;

1. MTEKNOLOJIA DAWA MSAIDIZI – NAFASI TATU (3)

A. KAZI NA MAJUKUMU YA MTEKNOLOJIA DAWA MSAIDIZI.

i. Kuainisha, kuandaa na kuagiza mahitaji ya dawa na vifaa tiba katika eneo lake la kazi.

ii. Kuuza dawa na vifaa tiba kwa wateja/wagonjwa.

iii. Kuhifadhi dawa na vifaa tiba.

iv. Kuelimisha jamii kuhusu matumizi sahihi ya dawa.

v. Kukagua dawa, vifaa tiba kemikali, vitendanishi na vipodozi katika Duka la Dawa la Hospitali.

vi. Kutoa taarifa juu ya madhara yatokanayo na matumizi ya dawa.

vii. Kushiriki kazi za kamati ya usimamizi wa Duka la Dawa la Hospitali.

viii. Kuandaa taarifa ya matumizi ya dawa na vifaa tiba.

ix. Kufanya uchunguzi wa ubora wa dawa, vifaa tiba kemikali, vitendanishi na vipodozi.

x. Kufanya kaguzi mbalimbali katika sehemu zinazohifadhi dawa.

xi. Kusimamia utendaji wa kazi watumishi walio chini yake.

xii. Kutunza kumbukumbu za dawa na vifaa tiba pamoja na taarifa za mwezi za Duka la Dawa.

xiii. Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake wa kazi zinazohusiana na elimu, uzoefu na ujuzi wake.

B. SIFA ZA MWOMBAJI.

Awe na Astashahada/Cheti (Certificate) katika fani ya Uteknolojia dawa wasaidizi kutoka Chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali na ambao wamesajiliwa na Baraza la Wafamasia.

C. MSHAHARA

Kwa kuzingatia waraka wa Serikali mshahara ni TGHS A.

MASHARTI YA KAZI/WAOMBAJI KWA UJUMLA

i. Awe raia wa Tanzania.

ii. Awe na umri wa kuanzia miaka 18 hadi 45

iii. Waombaji wote waambatanishe nakala ya cheti cha kuzaliwa.

iv. Awe na Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIN).

v. Nafasi ya Kazi inayoombwa iandikwe katika kichwa cha habari cha barua.

vi. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (a detailed C.V) yenye anuani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika pamoja na namba zao za simu.

vii. Maombi yote yaambatane na nakala za vyeti vya taaluma na mafunzo kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali:

- Cheti cha mtihani wa Kidato cha IV

- Cheti cha mafunzo (professional).

- Cheti cha kuzaliwa.

- Picha Moja “Passport Size” ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.

- Usajili kamili (Full Registration) au Leseni hai ya kufanya kazi ya taaluma husika.

viii. Asiwe Mwajiriwa wa Serikali au Mwajiriwa wa Hospitali za Mashirika ya Dini ambaye mshahara wake unalipwa na Serikali.

ix. Waombaji walioajiriwa kwa mkataba wa ajira kutoka kwa Wadau wa Maendeleo katika Sekta ya Afya wanatakiwa kuambatisha nakala za mkataba na barua za uthibitisho kutoka kwa Wakurugenzi wa Halmashauri husika.

x. Awe hajawahi kufukuzwa, kuacha kazi au kustaafishwa katika Utumishi wa Umma.

xi. “Testimonials”, “Provisional results”, “Statement of results”, hati za matokeo za kidato cha IV na VI (form IV and form Vi result slips) HAVITAKUBALIWA.

xii. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kughushi zitapelekea wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.

xiii. Nakala za vyeti vyote viwe vimethibitishwa (Certified copies).

xiv. Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 16/03/2023 saa 9:30 alasiri.

xv. Maombi yanaweza kuandikwa kwa lugha ya Kiswahili au Kiingereza na yatumwe kwa njia ya posta kwa anuani ifuatayo.

Barua zote zitumwe kwa anwani iliyopo hapa chini.

MKURUGENZI MTENDAJI,

HALMASHAURI YA WILAYA,

S.L.P 23,

LIWALE.

Aidha, barua za maombi zinaweza kuwasilishwa moja kwa moja katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale.

Limetolewa na;

MKURUGENZI MTENDAJI,

HALMASHAURI YA WILAYA,

LIWALE

TANGAZO LA KAZI IDARA YA AFYA.pdf

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO AWAMU YA PILI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025 February 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MKATABA MSF May 07, 2025
  • TANGAZO LA KUANZA KWA MFUMO MPYA WA TAUSI KWA AJILI YA UTOAJI HUDUMA YA MALIPO MBALIMBALI YA SERIKALI KWA NJIA YA MTANDAO February 20, 2023
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI October 09, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAPOKEA TUZO YA GLASS YA ELIMU KIMKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA KWANZA KWA MWAKA 2024

    May 02, 2025
  • UFUNGWAJI YA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA.

    November 01, 2024
  • MKUTANO WA KAWAIDA WA BARAZA LA HALMASHAURI

    October 30, 2024
  • UKAGUZI WA UTEKELEZAJI WA KUTENGWA, KUPIMWA NA KUMILIKISHA WAFUGAJI MAENEO RASMI KWAAJILI YA ZOEZI LA UFUGAJI KATIKA KATA YA KIMAMBI.

    October 25, 2024
  • Angalia Zote

Video

Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • www.tamisemi.go.tz
  • Kupata Hati ya Mshahara (Salary Slip) kwa Watumishi wa Umma
  • Bodi ya Ajira
  • Utabiri wa Hali ya Hewa
  • Taarifa za huduma ya elimu
  • Taarifa za huduma ya afya

Tovuti Linganifu

  • Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Linndi RS
  • Ruangwa
  • Nachingwea
  • Lindi Manispaa

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Dissertation-Writingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters

    Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE

    Simu ya Mezani: 023 2937043

    Mawasiliano ya mkononi:

    Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz

Anuani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.