• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Liwale District Council
Liwale District Council

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Uhasibu
      • Miundo Mbinu
      • Afya
      • Usafishaji na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Mifugo
    • Vivutio vya kitalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Ugani
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Uchumi na Mazingira
      • Community Services
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Miongozo mbalimbali
  • KItuo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi na kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Mlembwe

MRADI WA KUHIFADHI MAZINGIRA KIJIJI CHA NAMBINDA KATA YA MLEMBWE

MRADI wa Kuhifadhi Misitu kupitia biashara Endelevu ya mazao ya misitu unaotekelezwa na Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG) na Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu

(MJUMITA) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo na Ushirikiano la Uswis (SDC) umewabadilisha wananchi wa Kijiji cha Nambinda wilayani Liwale mkoani Lindi na sasa wameacha tabia ya kuhalibu misitu na wamejua thamani yake.

Wananchi wa Kijiji hicho wameanza kujua thamani ya misitu baada ya mashirika hayo kuwapa elimu ya ya shughuli za uzalishaji endelevu wa mazao yatokanayo na misitu na matumizi bora ya ardhi.

 Mzalishaji wa mbao wa kijiji hicho Hemed Kipaga akizungumza kwa niaba ya wenzake wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari ambao wapo katika ziara ya kujifunza kuhusu utekelezaji wa Usimamizi Shirikishi wa Misitu wilayani Liwale mkoani hapa waliotaka kujua hali ya utunzaji wa misitu ilivyokuwa kabla ya kupokea mradi huo alisema ilikuwa mbaya sana.

“Kwanza kabisa napenda kuyashukuru mashirika haya TFCG na MJUMITA kwa kutuletea mradi huu kwani tumeweza kufanikiwa mambo mengi, kabla ya mradi hatukuwa na matumizi bora ya ardhi ukataji wa miti ulikuwa wa hovyo hovyo tu mtu alipokuwa akijisia alikuwa akiingia msituni na kukata miti” alisema Kipaga.

Alisema baada ya kupata mradi huo wameweza kutenga maeeneo ya matumizi bora ya ardhi ambayo aliyataja kuwa ni ya makazi msongamano,eneo la kilimo na la kuhifadhi msitu na kuwa mpango huo umesaidia sana kuhifadhi misitu.

Awali akizungumza na waaandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, Tina Sekambo alisema halmashauri hiyo imetenga sh.30 milioni kwa ajili ya kusaidia utunzaji wa misitu na kuwa mabadiliko ya kiuchumi yamekuwa ni moja ya sababu ya wananchi katika baadhi ya maeneo ya wilaya hiyo kukata miti ya asili na kuanza kupanda mikorosho.

Mkuu wa Wilaya ya Liwale Judith Nguli alisema utunzaji wa miti ni jukumu la kila mwananchi na alitumia nafasi hiyo kuwaomba wadau mbalimbali kufika katika wilaya hiyo kusaidia utunzaji wa misitu na kuwa mtu yeyote atakaye bainika akihalibu misitu kwa namna yoyote atachukuliwa hatua za kisheria.

Nguli aliyashukuru mashirika yanayoisaidia serikali katika suala zima la uhifadhi wa misitu ya asili katika wilaya hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO AWAMU YA PILI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025 February 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MKATABA MSF May 07, 2025
  • TANGAZO LA KUANZA KWA MFUMO MPYA WA TAUSI KWA AJILI YA UTOAJI HUDUMA YA MALIPO MBALIMBALI YA SERIKALI KWA NJIA YA MTANDAO February 20, 2023
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI October 09, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI (BVR KIT) JIMBO LA LIWALE WAPATIWA MAFUNZO

    May 14, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAPOKEA TUZO YA GLASS YA ELIMU KIMKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA KWANZA KWA MWAKA 2024

    May 02, 2025
  • UFUNGWAJI YA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA.

    November 01, 2024
  • MKUTANO WA KAWAIDA WA BARAZA LA HALMASHAURI

    October 30, 2024
  • Angalia Zote

Video

Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • www.tamisemi.go.tz
  • Kupata Hati ya Mshahara (Salary Slip) kwa Watumishi wa Umma
  • Bodi ya Ajira
  • Utabiri wa Hali ya Hewa
  • Taarifa za huduma ya elimu
  • Taarifa za huduma ya afya

Tovuti Linganifu

  • Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Linndi RS
  • Ruangwa
  • Nachingwea
  • Lindi Manispaa

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Dissertation-Writingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters

    Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE

    Simu ya Mezani: 023 2937043

    Mawasiliano ya mkononi:

    Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz

Anuani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.