• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Liwale District Council
Liwale District Council

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Uhasibu
      • Miundo Mbinu
      • Afya
      • Usafishaji na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Mifugo
    • Vivutio vya kitalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Ugani
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Uchumi na Mazingira
      • Community Services
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Miongozo mbalimbali
  • KItuo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi na kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Liwale Kupatiwa Mabomu Baridi 700 ya Kupambana na Tembo

Imewekwa:: July 17th, 2024

Wilaya ya Liwale kupatiwa mabomu baridi 700 kwa ajili ya kupambana na wanyama waharibufu na wakali tembo ambao wamekuwa wakiharibu mazao na kuhatarisha maisha ya watu hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Dustun Kitandula (MB) wakati ikihutubia katika mkutano wa hadhara viwanja vya Nanjinji Liwale Mjini.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Dustun Kitandula amefanya ziara katika Wilaya ya Liwale na kuanza kwa kufanya kikao cha ndani cha watendaji na badae kuongea na wananchi wa Liwale ambapo amewaeleza nia ya Serikali katika kupambana na wanyamapori ambao ni waharibifu tembo ikiwemo kuleta mabomu baridi 700 ambayo yatasaidia kupambana na tembo Na kutoa mafunzo mbalimbali na kununua vifaa vya kisasa kwa ajili ya kuzuia tembo.

Mheshemiwa Kitandula amesemakuwa Serikali kupitia Wizara umeunda mpango aikiwemo kuhakikisha Wilaya ya Liwale inaangaliwa kwa jicho la utaofauti ikiwemo kuongeza vifaa mbalimbali ikiwemo ndege nyuki, kuwafunga kola za kidigitali tembo ambao wapo kwenye makundi ili kuweza kufatilia nyendo zao na pia kuongeza idadi ya vijana ambao watapatiwa mafunzo ya kukabiliana na tembo katika vijiji vyao kwa sababu eneo la Wilaya ya Liwale ni kubwa na changamoto ni kubwa.

Mheshimiwa Kitandula ameendelea kuwasisitiza wananchi kuwa Serikali itaendelea kuchukua hatua madhubuti za kupambana na wanyama hawa kwani kupitia bajeti hii ya mwaka wa fedha itihakikisha vifaa mbalimbali vita nunuliwa na kuongeza nguvu kazi katika eneo la Liwale na kutoa  mbinu mbalimbali za kupambana na wanyama hawa ikiwemo kutumia matofali ya pilipili, senyenge, sauti za kukera, na diseli chafu yenye kutoa harufu njia hizi zitasaidia kupunguza wanyama hawa kuvamia maeneo ya watu hivyo ametoa wito kwa wananchi kutumia mbinu hizo.

Pia Mheshimiwa Waziri Kitandula amesema Serikali itahakikisha inachimba mabwawa katika hifadhi  zote na mapori ili kuhakikisha tembo hawa wanapata maji hukohuko katika makazi yao na kucha kuja kwenye makazi ya watu na pia ametoa rai kwa wananchi kuacha kilimo cha kuhamahama kwani watu wengi wamekuwa wakilima katika hifadhi na hivyo kusababisha tembo kuhama kwenye makazi yao  na pia idadi kubwa ya makundi ya Ngombe yamekuwa yakichangia kusababisha kero hii hivyo Mkuu wa Wilaya endelea kupambana na mifugo hii ili tuondoe changamoto hii.

Kwa upande mwingine wa kulipa fidia na kifuta machozi  kwa waathirika wa wanyama waharibifu Mheshimiwa Waziri Kitandula amesekuwa mpaka sasa Serikali imefanikisha kurekebisha kanuni ambazo zilikuwa zinatumika kufanya tathimini na kulipa hivyo kuanzia sasa kanuni hizi zimeboreshwa na kuongezwa ukilinganisha na hapo awali  na madeni yote ambayo wizara inadaiwa italipa kwa waathirika wote wa wanyama waharibifu na mazao ambayo yatakuwa yameharibiwa pia  kwa upande wa Wilaya ya  Liwale katika kipindi cha mwaka 2020 hadi 2024, watu 17 waliuawa na 3 kujeruhiwa na wanyama wakali na waharibifu ambapo kati yao watu 16 wamelipwa jumla ya Tshs 14,500,000.

Aidha katika mgogoro kati ya jumuiya Magingo na TANAPA Mheshimiwa Waziri amesema kuwa wizara itashughulikia kwa kutuma wataalamu ambao watakuja na kukagua mipaka upya na kuangalia na kisha pande zote zitakaa ili kuweza kumaliza mgogoro huu.





Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO AWAMU YA PILI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025 February 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MKATABA MSF May 07, 2025
  • TANGAZO LA KUANZA KWA MFUMO MPYA WA TAUSI KWA AJILI YA UTOAJI HUDUMA YA MALIPO MBALIMBALI YA SERIKALI KWA NJIA YA MTANDAO February 20, 2023
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI October 09, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HISTORIA IMEANDIKWA, HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAFANYA VIZURI KWA 100% KATIKA MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI (BVR KIT) JIMBO LA LIWALE WAPATIWA MAFUNZO

    May 14, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAPOKEA TUZO YA GLASS YA ELIMU KIMKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA KWANZA KWA MWAKA 2024

    May 02, 2025
  • UFUNGWAJI YA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA.

    November 01, 2024
  • Angalia Zote

Video

Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • www.tamisemi.go.tz
  • Kupata Hati ya Mshahara (Salary Slip) kwa Watumishi wa Umma
  • Bodi ya Ajira
  • Utabiri wa Hali ya Hewa
  • Taarifa za huduma ya elimu
  • Taarifa za huduma ya afya

Tovuti Linganifu

  • Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Linndi RS
  • Ruangwa
  • Nachingwea
  • Lindi Manispaa

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Dissertation-Writingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters

    Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE

    Simu ya Mezani: 023 2937043

    Mawasiliano ya mkononi:

    Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz

Anuani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.