• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Liwale District Council
Liwale District Council

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Uhasibu
      • Miundo Mbinu
      • Afya
      • Usafishaji na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Mifugo
    • Vivutio vya kitalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Ugani
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Uchumi na Mazingira
      • Community Services
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Miongozo mbalimbali
  • KItuo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi na kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

MSF Yakarabati Majengo Hospitali ya Wilaya Liwale

Imewekwa:: January 26th, 2024

Katibu Tawala wa Wilaya ya Liwale Ndugu Azilongwa Mwinyimvua Bohari amezindua majengo ya hospitali ya Wilaya ya Liwale ambayo yamekarabatiwa na Shirika la Madaktari wasio kuwa na Mipaka (MSF) ambapo jumla ya kiasi cha shilingi milioni 149,935,995 zimetumika kukarabati jengo la mama na mtoto, jengo la upasaji wodi ya wazazi pamoja na kichomea taka.

Katibu Tawala Bi Bohari amemshukukuru Mkurugenzi wa Shirika la madaktari wasiokuwa na mipaka kwa ukarabati ambao wameufanya katika hospitali ya Wilaya ya Liwale katika majengo haya kwani ni kazi kubwa imefanyika majengo haya yatasaidia kutoa huduma bora za afya kwa mama wajawazito na watoto wachanga.

Aidha Bi Bohari ameliomba Shirika hilo kupitia kwa Mkurugenzi wake Stephani Cornish  kuongeza mkataba ili waendelee kutoa huduma za afya  kwa wananchi wa wilaya ya Liwale hususa wakina mama na watoto kwa sababu hawa ndio wanufaika wakubwa wa huduma hii na pia Wilaya yetu ni kubwa na ina vijiji vingi tunawapongeza kwa sababu mmeweza kuwafika mpaka watu wa vijijini na kuwapa huduma  na pia Serikali itaendelea kushirikiana na nyie kwa kila hatua hivyo tunawapongeza kwa kazi kubwa ambayo mnaifanya kwani mmeweza kutusaidia kutoa madawa, watumishi na huduma nyingine muhimu hivyo tunawashukuru sana.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika hilo Bwana Stephan Cornish amesama kuwa Shirika la Madaktari Wasiokuwa na Mipaka waliona inafaa kuichagua Wilaya ya Liwale kutokana na changamoto ya watoto wengi na wamama wajawazito kupoteza maisha hivyo wakaona ni vyema kuileta huduma hii katika Wilaya ya Liwale ili kuweza kupunguza na kumaliza kabisa changamoto hii.

“Na leo hii tumejionea wenyewe ukarabati mkubwa ambao umefanywa na shirika hili tumejionea hodi bora kabisa. Majengo mapya kabisa na vifaa vyake ikiwemo jengo la upausuaji pamoja na wodi na lengo letu ni kuhakikisha tunarejesha tabasamu kwa mama wajawazito na watoto wajifungue salama na kupata huduma bora na kufurahi” hata hivyo tunawajibu wakuendelea kufanya kazi na kutoa huduma katika hospitali na vituo vyote vya afya ili watoto na mama wajawazito wafurahie huduma na pia tunaishukurua Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kuendelea kushirikiana na sisi kwa ukaribu zaidi.

Aidha Mganga Mkuu wa Mkoa wa Lindi Ndugu Heri kagya amewashukuru wadau hawa madaktari wasiokuwa na mipaka kwa kuendelea kusaidia kutoa huduma hizi za afya hususa kwa mama wajawazito na watoto kwani huduma ambazo zinatoewa ni za ubora kabisa wadau hawa wanatusaidia katika kutoa huduma, kuongeza idadi ya watumishi kwa kuwaajiri na kutoa dawa ambazo zina wasaidia watu wetu hawa hususa hapa Liwale.

Hata hivyo Serikali ipo tayari kushirikiana na nyie wadau wetu  na pia tunatamani kuona mnaongeza miradi mingine katika maeneo yetu mengine ya Mkoa wa Lindi ili kuongeza wigo wa utoawaji wa huduma hususa kwa mama wajawazito na watoto wa changa  na pia tumeona mchango wenu mkubwa katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora umekuwa mstari wa mbele katika kutoa chanjo mbalimbali kwa watoto wadogo dhidi ya magonjwa ya mlipuko na kutusaidia katika tafiti mbalimbali tunaomba tundelee kushirikiana na Serikali iko tayari kushirikiana na nyie kwa ukaribu .

Kwa upande mwingine Kaimu  Mganga Mkuu  wa Wilaya ya Liwale  Dactari Khadija Kitiku amewashukuru wadau hawa wa madactari wasio kuwa na mipaka kwa msaada wao ambao wanautoa  kwa kuwapa huduma bora  mama wajawazito na waatoto hususa kwenye  vituo vya afya vya vijijini ikiwemo Kimambi, Kibutuka, Lilombe ambavyo vipo mbali na hospitali tunawashukuru kwa msaada wao huu na pia niwaombe wasiishie hapo tu pia tunaomba watusaidie  kuatatua changamoto nyingi ambazo bado tunazo hapa ikiwemo kuongeza watumishi wa afya hususa katika hospitali ya wilaya mpya, jenereta la uwakika  ili kuweza kutoa huduma bora ambazo tumezikusudaia kuwapa na pia kupunguza na kumaliza kabisa vifo vitokanavyo na uzazi hasa mama wajawazito na watoto hapa Liwale.





Baadhi ya picha Mbalimbali katika uzinduzi wa Majengo yaliyo karabatiwa na MSF shirika la madaktari wasio na mipaka na vifaa tiba mbalimbali katika Hospitali ya Wilaya ya Liwale.

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO AWAMU YA PILI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025 February 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MKATABA MSF May 07, 2025
  • TANGAZO LA KUANZA KWA MFUMO MPYA WA TAUSI KWA AJILI YA UTOAJI HUDUMA YA MALIPO MBALIMBALI YA SERIKALI KWA NJIA YA MTANDAO February 20, 2023
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI October 09, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HISTORIA IMEANDIKWA, HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAFANYA VIZURI KWA 100% KATIKA MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI (BVR KIT) JIMBO LA LIWALE WAPATIWA MAFUNZO

    May 14, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAPOKEA TUZO YA GLASS YA ELIMU KIMKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA KWANZA KWA MWAKA 2024

    May 02, 2025
  • UFUNGWAJI YA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA.

    November 01, 2024
  • Angalia Zote

Video

Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • www.tamisemi.go.tz
  • Kupata Hati ya Mshahara (Salary Slip) kwa Watumishi wa Umma
  • Bodi ya Ajira
  • Utabiri wa Hali ya Hewa
  • Taarifa za huduma ya elimu
  • Taarifa za huduma ya afya

Tovuti Linganifu

  • Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Linndi RS
  • Ruangwa
  • Nachingwea
  • Lindi Manispaa

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Dissertation-Writingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters

    Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE

    Simu ya Mezani: 023 2937043

    Mawasiliano ya mkononi:

    Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz

Anuani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.