• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Liwale District Council
Liwale District Council

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Uhasibu
      • Miundo Mbinu
      • Afya
      • Usafishaji na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Mifugo
    • Vivutio vya kitalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Ugani
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Uchumi na Mazingira
      • Community Services
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Miongozo mbalimbali
  • KItuo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi na kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

ZIARA YA MKUU WA WILAYA KATA YA KICHONDA

Imewekwa:: July 18th, 2023

Ziara ya Mkuu wa Wilaya Kata ya Kichonda 

Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodalack Mlinga ametembelea Kata ya Kichonda yenye jumla ya Vijiji vitatu ambavyo ni Mbuli, Nyela, na Kichonda na kukagua Miradi mbalimbali ya maendeleo na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi.

Katika ziara iyo Mkuu wa Wilaya alitembelea vijiji vyote ikiambatana na wataalamu kutoka idara tofauti na kufanya mikutano nakusikiliza kero zinazo wakabili wananchi wa maeneo hayo na kuzitolea ufafanuzi kwa wananchi

Miongoni mwa kero zilizo wasilishwa kwa Mkuu wa Wilaya katika Kata ya Kichonda ni kuwepo na shida ya upatikanaji wa Maji katika Kata ya Kichonda na hivyo kusababisha wananchi kutumia maji ambayo siyo safi na salama na hata ivyo kufuata maji umbali mrefu ambayo yanatumiwa na mifugo pia.

Ubovu wa barabara kutoka Nyela mpaka Mbuli kwenda Liwale wananchi wamemueleza Mkuu wa Wilaya changamoto ya barabara imekuwa ni kero kwao sababu barabara iyo imekuwa ikitumika kusafirisha mazao kutoka shamabani kwenda kwenye maghala na hivyo kumuomba awasaidie ili iweze kupitika katika vipindi vyote ili iweze kurahisisha usafiri.

Wanyama waribifu tembo imekuwa ni changamoto kwa wananchi wa Kata ya Kichonda na hivyo kumuomba Mkuu wa Wilaya kuwasaidia pindi wanapo haribu mazao yao kuwasaidia kupata vifuta jasho na pia kuwasaidia kwa kuwatumia askari wa Wanyamapori kuwatoa katika maeneo yao nakuwarudisha kwenye hifadhi.

Pia wamemuomba Mkuu wa Wilaya kutatua kero ya Mawasiliano kwani katika Kata ya Kichonda na Vijiji vyake kumekuwa na changamoto ya kukosekana kwa mawasiliano hivyo wamemuomba mkuu wa wilaya kuhakikisha wanapata minara ya simu ili kurahisisha mawasiliano katika Kata yao na Vijiji vyao.

Kwa upande wa Pembejeo ni miongoni mwa kero ambayo imewasilishwa kwa Mkuu wa Wilaya kuwa kunabadhi ya watu wameenza kupata Pembejo na wengine awajapata Pembejeo hizo kutokana na kutosomeka kwenye mfumo na hivyo baadhi yao kukosa Pembejeo hizo na ukiangalia kwa sasa ni msimu wa upuliziaji wa Mikorosho ivyo wamemuomba Mkuu wa Wilaya kuwasaidia kutatua changamoto iyo.

Aidha katika kutolea majibu ya kero ya maji Meneja wa maji Wilaya ya Liwale ndugu Rumbika Wegoro amesema kuwa” kwa Kata ya Kichonda kumekuwa na tatizo la watu kuaribu na kukata miundombinu ya maji jambo linalopelekea kukosekana kwa maji katika Kata ya Kichonda na hivyo kuwataka wanachi kutunza miundombinu iyo ili iweze kuwasidia kupata maji safi na salama.”.

Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Mlinga baada ya kusikiliza kero na kuzitolea ufafanuzi alitoa Maagizo kwa wataalamu na watendaji wote wa Kata ya Kichonda  kuwa watu wote wanao haribu miundombinu ya maji kwa kukata mabomba Meneje wa maji kwa kushirikiana na watendaji wengine ni lazima wafanye uchunguzi ili kuwabaini wanao hujumu na kuwachukulia hatua stahiki.

Pia ametoa agizo kwa Maafisa Ugani wote kuhakikisha wanawagawia wakulima wote ambao wamesajiliwa Pembejeo zao kwa wakati na kama kunachangamoto nyingine basi zifanyiwe kazi kwa haraka ili mkulima apate Pembejeo zake kwani pembejeo hizo zinatolewa bure na Serikali.

Mkuu wa Wilaya amegiza kuwa wanachi wote ni lazima wajitolee kwa kwenye miradi ya maendelo ikiwemo Shule ya Sekondari ya Kichonda ambayo ujenzi wake unaanza sasa na pia wanachi wazawa wepewe kazi ambazo azihitaji wataalamu hivyo wawe kipaumbele na si kutoka sehemu nyingine. Pia ametoa agizo kwa Vyombo kuhakikisha wanafuatilia suala la uzwaji wa ardhi kiholele na kudhibiti hali hiyo katika Kata ya Kichonda.





Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO AWAMU YA PILI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025 February 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MKATABA MSF May 07, 2025
  • TANGAZO LA KUANZA KWA MFUMO MPYA WA TAUSI KWA AJILI YA UTOAJI HUDUMA YA MALIPO MBALIMBALI YA SERIKALI KWA NJIA YA MTANDAO February 20, 2023
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI October 09, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HISTORIA IMEANDIKWA, HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAFANYA VIZURI KWA 100% KATIKA MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI (BVR KIT) JIMBO LA LIWALE WAPATIWA MAFUNZO

    May 14, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAPOKEA TUZO YA GLASS YA ELIMU KIMKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA KWANZA KWA MWAKA 2024

    May 02, 2025
  • UFUNGWAJI YA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA.

    November 01, 2024
  • Angalia Zote

Video

Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • www.tamisemi.go.tz
  • Kupata Hati ya Mshahara (Salary Slip) kwa Watumishi wa Umma
  • Bodi ya Ajira
  • Utabiri wa Hali ya Hewa
  • Taarifa za huduma ya elimu
  • Taarifa za huduma ya afya

Tovuti Linganifu

  • Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Linndi RS
  • Ruangwa
  • Nachingwea
  • Lindi Manispaa

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Dissertation-Writingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters

    Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE

    Simu ya Mezani: 023 2937043

    Mawasiliano ya mkononi:

    Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz

Anuani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.