• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Liwale District Council
Liwale District Council

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Uhasibu
      • Miundo Mbinu
      • Afya
      • Usafishaji na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Mifugo
    • Vivutio vya kitalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Ugani
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Uchumi na Mazingira
      • Community Services
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Miongozo mbalimbali
  • KItuo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi na kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

Mheshimiwa Mlinga Mtengua Mwenyekiti wa Kijiji cha Kipelele

Imewekwa:: December 1st, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga amemtengua Mwenyekiti wa kijiji cha Kipelele Ndugu abruhaman Abdallah Mnoile kwa tuhuma za kuongoza uzwaji wa ardhi kiholelea bila kuchukua hatua yoyote kwa wahusika jambo linalopelekea kuibuka kwa migogoro ya ardhi katika kijiji hicho aidha Mheshimiwa Mlinga Ameteuwa Bi Salma Haji kuwa mwenyekiti wa Kijiji cha Kipelele.

Hayo yamejiri katika ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga baada ya wananchi kukerwa na mwenendo huo wakuuza ardhi bila kufuta utaratibu ambao upo hata hivyo Mheshimiwa Mlinga amevitaka vyombo vinavyo husika ikiwemo Polisi na Takukuru kuchunguza walio husika katika kuuza maeneo hayo na wachukuliwe hatua za kisheria ikiwemo kuwapeleka Mahakamani na pia amewataka viongozi wa kijiji cha Kipelele na Ngumbu kumaliza kero zao za mipaka kabla ya January mosi

Hata hivyo Mheshimiwa Mlinga amewataka wananchi kuwa mstari wa mbele katika kuisimamia Serikali ya kijiji ili kuweza kudthibiti mambo kama haya yasitokee kwani kuuza ardhi bila kufuta utaratibu ni kosa na hivyo “wale wote ambao pia wamenunua maeneo hapa Kipelele bila kufuta utaratibu wametapeliwa hivyo watoe ushirikiano kwa serikali na vyombo ili tuwabaini wahusika mrudishiwe pesa zenu hayo ameyasema Mheshimiwa Mlinga”.

Aidha Mheshimiwa Mlinga amewakumbusha wafugaji ambao wapo na wamenunua maeneo katika kijiji cha Kipelele  kuwa eneo hilo sio kwa ajili ya mifugo bali ni kwajili  ya shughuli nyingine hivyo ni bora wakaondaka haraka ili kuepusha matatizo watakayo yapata kwani wafugaji wamekuwa wakilisha mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima  na hivyo kuwataka warudi kwenye maeneo yao sambamba na hilo pia Mheshimiwa Mlinga amewaeleza wananchi wa Kipelele kuwa Serikali bado inafanyia kazi kuwepo kwa wanyama waharibifu  ikiwemo kutoa mafunzo na pia kuna mradi mpya wa GIZ kutoka Serikali ya Ujerumani ambapo watotaoa mafunzo kwa vijiji ili tuweze kukabilina na wanyama hao .

Pia Mheshimiwa Mlinga amemtaka Mkurugenzi kuhakikisha anasimamia na kumalizika kwa Wakati  kituo cha afya cha Naujombo kilichopo Kata ya Mirui ili wananchi waweze kupata huduma za kitabibu katika maeneo yao na pia amewakumbusha watumuishi wa umma kukumbuka wajibu wao wakutoa huduma kwa wananchi kwa wakati na kuondoa changamoto kwa wananchi na pia watumishi wote wakae maeneo yao ya kazi ni marufuku kwenda kudhurula mjini bila kibali mbaki vituoni mtoe huduma kwa wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Liwale Mheshimiwa Goodluck Mlinga akikagua kituo cha afya cha Naujombo Kata ya Mirui.


Muonekano wa kituo cha afya cha Naujombo

Matangazo

  • TANGAZO LA MIKOPO AWAMU YA PILI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025 February 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MKATABA MSF May 07, 2025
  • TANGAZO LA KUANZA KWA MFUMO MPYA WA TAUSI KWA AJILI YA UTOAJI HUDUMA YA MALIPO MBALIMBALI YA SERIKALI KWA NJIA YA MTANDAO February 20, 2023
  • TANGAZO LA MNADA WA MAGARI NA PIKIPIKI October 09, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • HISTORIA IMEANDIKWA, HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAFANYA VIZURI KWA 100% KATIKA MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI (BVR KIT) JIMBO LA LIWALE WAPATIWA MAFUNZO

    May 14, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAPOKEA TUZO YA GLASS YA ELIMU KIMKOA KWA KUSHIKA NAFASI YA KWANZA KWA MWAKA 2024

    May 02, 2025
  • UFUNGWAJI YA MAFUNZO YA JESHI LA AKIBA.

    November 01, 2024
  • Angalia Zote

Video

Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • www.tamisemi.go.tz
  • Kupata Hati ya Mshahara (Salary Slip) kwa Watumishi wa Umma
  • Bodi ya Ajira
  • Utabiri wa Hali ya Hewa
  • Taarifa za huduma ya elimu
  • Taarifa za huduma ya afya

Tovuti Linganifu

  • Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Linndi RS
  • Ruangwa
  • Nachingwea
  • Lindi Manispaa

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Dissertation-Writingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters

    Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE

    Simu ya Mezani: 023 2937043

    Mawasiliano ya mkononi:

    Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz

Anuani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.