• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Liwale District Council
Liwale District Council

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Liwale

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Uhasibu
      • Miundo Mbinu
      • Afya
      • Usafishaji na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA na Takwimu
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ufugaji wa Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Mifugo
    • Vivutio vya kitalii
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Ugani
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Utawala Mipango na Fedha
      • Uchumi na Mazingira
      • Community Services
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Mheshimiwa Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu
    • Miongozo mbalimbali
  • KItuo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shughuli za ofisi na kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha

WANAWAKE, VIJANA, WAZEE NA WENYE ULEMAVU KUFAIDIKA NA ASILIMIA 30 YA ZABUNI ZA SERIKALI

Imewekwa:: September 9th, 2025

Taasisi isiyo ya kiserikali ya WAJIBU kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), imeendesha mafunzo kwa makundi maalumu katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, mkoani Lindi.

Mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha washiriki kufahamu Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2023 na kanuni zake, ambazo zinaelekeza taasisi za ununuzi kutenga asilimia 30 ya bajeti ya mwaka kwa ajili ya makundi maalumu kushiriki katika zabuni za umma. Makundi hayo ni wanawake, vijana, wazee na watu wenye ulemavu.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Afisa Ununuzi kutoka TAMISEMI, Bw. Amiri Mhando, aliwahimiza washiriki kutumia ipasavyo fursa zilizopo, ikiwemo mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. Aliongeza kuwa, TAMISEMI imeanza mchakato wa kutafuta uwezekano wa taasisi za umma kutoa kianzio cha kazi (advance payment) kwa makundi yatakayopata zabuni, ambacho kitarejeshwa baada ya mauzo.

Kwa upande wake, Afisa Ununuzi kutoka PPRA, Bi. Tumpe Ngalla, alisema mpango huo unalenga kutoa fursa sawa kwa makundi maalumu kushiriki katika biashara za serikali na kuchangia ukuaji wa uchumi wa wananchi. Naye Afisa Tehama wa PPRA, Bw. Damas Makweba, aliwahimiza washiriki kuhakikisha wanajisajili rasmi katika mfumo wa NeST ili kushindania zabuni zinazotolewa na taasisi za umma.

Afisa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka WAJIBU, Bi. Tekla Mleleu, alishukuru mwamko wa makundi maalumu kushiriki mafunzo hayo na kubainisha kuwa WAJIBU ni taasisi isiyo ya kiserikali yenye lengo la kuinua jamii kupitia kukuza uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa fedha za umma.

Aidha, alifafanua kuwa kupitia ufadhili wa Balozi za Norway na Sweden, WAJIBU imeshirikiana na PPRA pamoja na Ofisi ya Rais – TAMISEMI kuwezesha mafunzo hayo kwa makundi maalumu, huku akiwahimiza washiriki kutumia ipasavyo fursa hiyo kujifunza mfumo wa NeST na namna ya kushiriki katika zabuni za umma kupitia wakufunzi wa PPRA na OR-TAMISEMI.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 12, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 24, 2025
  • MAKALA YA MAFANIKIO YA HUDUMA ZA JAMII NA MIUNDOMBINU NDANI YA MIAKA 61 YA UHURU WILAYA YA LIWALE. December 07, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MKATABA MSF May 07, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WANAWAKE, VIJANA, WAZEE NA WENYE ULEMAVU KUFAIDIKA NA ASILIMIA 30 YA ZABUNI ZA SERIKALI

    September 09, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YATOA JUMLA YA MKOPO WA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 773,523,370.00 KWA VIKUNDI 201 VYA WANAWAKE,VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

    June 08, 2025
  • HISTORIA IMEANDIKWA, HALMASHAURI YA WILAYA YA LIWALE YAFANYA VIZURI KWA 100% KATIKA MIRADI ILIYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025.

    May 30, 2025
  • WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA NA WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI (BVR KIT) JIMBO LA LIWALE WAPATIWA MAFUNZO

    May 14, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video nyingine

Viunganishi vya Haraka

  • OR - Tamisemi
  • Kupata Hati ya Mshahara (Salary Slip) kwa Watumishi wa Umma
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Utabiri wa Hali ya Hewa
  • Taarifa za huduma ya elimu
  • Taarifa za huduma ya afya

Tovuti Linganifu

  • Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Lindi RS
  • Ruangwa
  • Nachingwea
  • Lindi Manispaa

Watazamaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Dissertation-Writingservice.com

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Along Nachingwea Road opposite DDD Quarters

    Sanduku la Posta: P.O. BOX 23 LIWALE

    Simu ya Mezani: 023 2937043

    Mawasiliano ya mkononi:

    Baruapepe: ded@liwaledc.go.tz

Anuani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Hakimiliki 2023 © Halmashauri ya Wilaya ya Liwale. Haki zote zimehifadhiwa.